Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Dkt.
Faustine Ndugulile ametoa kauli hiyo leo alipokuwa akizungumza na wafanyakazi wa
Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) mkoani Arusha alipokutembelea taasisi za
wizara hiyo na kusema kuwa ni vyema
mamlaka hiyo ikajikita zaidi kutoa Elimu kwa jamii kwani ni kosa kisheria
kuendesha vyombo vya habari vya kimtandao (blogu na TV) bila kusajiliwa.
Waziri amewataka TCRA kupunguza gharama za usajili wa blogu na TV za mtandaoni ili vijana
waweze kujiajiri kupitia mitandao hiyo ambapo alitoa muda wa mwezi mmoja kuhakikisha sheria zote zimepitiwa na usajili kuendelea tena baada ya kusitishwa.
Katika hatua nyingine Waziri alitumia nafasi hiyo kuwaasa
mafundi simu wote wenye tabia za kufuata namba ya kipekee inayotambulisha simu
husika (IMEI) wanapopelekewa simu kwa ajili ya matengenezo na
kuwaasa kuwa watachukuliwa hatua za kisheria.
“Baadhi ya mafundi
simu wasio waaminifu wanatumika kufuta IMEI (International Mobile Equipment
Identity) namba za simu za mkononi za wateja wao ili simu hizo ziweze kutumika
tena kitendo ambacho ni kosa kisheria na serikali itawachukulia hatua kali mafundi
watakaobainika kufanya tabia hiyo” alisema Ndugulile.
Kwa upande wake meneja wa mamlaka ya Mawasiliano Kanda ya Kaskazini, Mhandisi Emelda Salumu
alisema kuwa mamlaka ya mawasiliano Tanzania kwa upande wa Kanda hiyo kwa mwaka
wa fedha 2020/2021 wana mpango wa kukusanya kiasi cha shilingi billioni 1.27 ambapo hadi sasa wamekusanya kiasi cha zaidi ya shilingi millioni 800.
Alisema katika kuhakikisha uhalifu kupitia mitandao ya simu unapungua wameamua
kutoa elimu kwa wananchi pamoja na mafundi simu ambapo jumla ya mafundi 332 wamepatiwa mafunzo kwa upande wa Kanda ya kaskazini ambapo kwa upande wa Kilimanjaro jumla ya mafundi 67
wamepatiwa mafunzo, Arusha 133, Tanga 67 na Manyara 78 ambapo kwa Manyara bado wapi kwenye
mafunzo.
“Mafunzo haya yatawasaidia kuwa wafanisi Katika kazi zao pia wataona utofauti
yao waliopewa mafunzo pamoja na wale ambao hawakupewa mafunzo.” Alisema.
Leave a comment