
Kampuni ya Twitter imepuuza agizo la Waziri Mkuu wa India Narendra Modi
la kuzifungia akaunti za Twitter ambazo anadai zinachochea maandamano ya
Wakulima wanaolalamikia Sheria kuwakandamiza na kuwapa faida Wafanyabiashara.
Serikali ya Waziri Mkuu Narendra Modi ilitaka twitter iondoe akaunti
zipatazo 1,100 na machapisho yanayosambaa mtandaoni yanayodai uongozi
unawanyonya wakulima na kuongeza kuwa baadhi ya akaunti zinafadhiliwa na maadui
zake kutoka Pakistan.
Licha ya kuwa hapo awali Mtandao huo wa kijamii uliondoa baadhi ya
akaunti mapema wiki iliyopita, Twitter imesema inaamini agizo hilo linakiuka
Sheria za India za Watu kuwa na uhuru wa kutoa maoni hivyo hawatozifungia.
Akielezea uamuzi wake katika chapisho la blogi, Mtandao wa twitter
umeweka wazi kuwa uamuzi wake ni kwa lengo la "ni kutunza misingi na
kutetea uhuru wa kujieleza".
Twitter imeripotiwa kuzifungia account zinazozidi 500 lakini ikaziacha
zile za Wanaharakati, Waandishi na za Wanasiasa.
Wakulima nchini India wamekuwa wakiandamana nje ya mji mkuu, New Delhi,
kutaka mageuzi ya kilimo tangu Novemba 26, licha ya kukumbana na vizuizi vya
polisi.
Polisi wamesema maafisa 300 wamejeruhiwa tangu kuanza kwa maandamano
hayo huku mamia ya waandamanaji wakiripotiwa kujeruhiwa na kifo cha mkulima
mwenye umri wa miaka 26 ambaye trekta lake lilipinduka baada ya kugonga kizuizi
cha polisi.
Serikali imeamua kuzima mtandao katika maeneo ya nchi hiyo ikiwa ni
juhudi za kuzuia maandamano, hatua inayotumiwa mara kwa mara kuzuia wapinzani.
Leave a comment