
Serikali ya Oman imetoa orodha ya nchi 10
ambazo zimezuliwa kuingia nchini humo chini ya uamuzi wa hivi karibuni
uliopitishwa na Kamati Kuu ya kushughulikia janga la corona.
Nchi zilizopigwa marufuku ni Tanzania, Afrika
Kusini, Lebanon, Sudan, Brazil, Nigeria, Guinea, Ghana, Sierra Leone, na
Ethiopia.
Marufuku hiyo itaanza kutekelezwa usiku wa
Alhamisi wiki hii na itadumu kwa siku 15
Hatua hiyo imetokana na maamuzi yaliyotolewa
na kamati ya udhitibi wa corona nchini humo.
Marufuku hiyo pia inawahusisha watu watakaopita katika nchi hizo ndani ya siku 14 kabla ya kuingia Oman ikiwa ni sehemu ya juhudi za kulinda raia wao dhidi ya corona.
Februari 15, Waziri wa Afya wa Oman alisema nchi yake inafikiria kuzuia safari za ndege kutoka kutoka nchi zinazoonesha kuwa na kiwango cha juu cha maambukizi ya virusi vya corona ikiwa ni baada ya kuthibitisha takwimu za maambukizi ya Corona kwa wasafiri wanaotokea nchini Tanzania kuwa katika kiwango cha juu sana, ambapo asilimia 18 ya wasafiri walikutwa na maambukizi ya virusi hivyo.
معاليه يؤكد أن بيانات القادمين من جمهورية تنزانيا للسلطنة سجلت فحوصات إيجابية بنسبة ١٨ بالمائة وهو رقم مرتفع جدا لذلك فإن اللجنة تدرس إيقاف رحلات القادمين من الدول التي ثبت للسلطنة أن لديها نسبة عالية من الإصابات
— وكالة الأنباء العمانية (@OmanNewsAgency) February 15, 2021
Kwa mujibu wa vyombo vya habari vya Oman, mkutano wa kamati hiyo uliongozwa na Waziri wa Mambo ya Ndani wa Oman Hammoud bin Faisal Al Busaid.
Leave a comment