
Klabu ya Namungo FC
imekwama kwa mara ya pili sasa kurejea nchini Tanzania kutokana na
kuahirishwa kwa mchezo wake dhidi ya CD De Agosto kutoka katika mji wa
Luanda nchini Angola.
Taarifa za awali
zilieleza kuwa timu hiyo ilipaswa kurejea nchini mapema Jumamosi Lakini mamlaka
nchini Angola zilisitisha safari hiyo zikidai kuwa marubani wa ndege ya
kukodi ambayo ilipaswa kuwasafirisha wachezaji hao walitakiwa wapumzike.
Hata
hivyo klabu hiyo kutoka kusini mwa Tanzania ilitarajiwa kuanza rasmi safari
yake ya kurejea Dar es salaam mapema leo lakini safari hiyo imekabiliwa na
mkwamo kutokana na watu watatu kukutwa na virusi vya corona na kuwekwa katika
karantini nchini humo ambapo mamlaka zimewazuia watu hao kuondoka.
Mwenyekiti
wa timu hiyo, Hassan Zadidu amewataka Watanzania kuiombea kwani inakumbana na
changamoto ambazo kwao ni ngumu kuzikabili kutokana na mazingira huku akidai
kuwa suala la wachezaji wawili na afisa mmoja katika msafara huo
kukutwa na virusi vya corona ni la uzushi
“Lakini
kwa bahati mbaya sana kitu wanachotumia ni cha uongo wanasema wamewapima test
ya kwanza wako positive lakini wanasema wamewapima test ya pili wako positive
lakini tulipowauliza kwa njia ya simu wakasema hawajawapima kwa mara ya pili
kwahiyo ni uongo tu na udanganyifu,” amesema Zadidu.
Baadhi
ya wachezaji wamesema kuwa hawakupata chakula chochote tangu walipowasili zaidi
ya maji na matunda huku wakidai kuwa wanateseka na kupitia katika mazingira
magumu
Shirikisho
la soka Barani Afrika CUF liliahirisha mchezo wa kombe la Shirikisho baina ya
timu hizo mbili uliopangwa uchezwe Jumapili ya tarehe 14 February mwaka huu,
kutokana na msafara wa timu ya Namungo kutakiwa kukaa karantini kutokana na
kadhia hiyo CAF Imesema kuwa italifikisha suala hilo kwenye kamati husika kwa ajili
ya uamuzi.
Klabu
ya Namungo iliingia katika hatua ya makundi ya kombe la Shirikisho baada ya
ushindi wa Agregate ya 5-3 dhidi ya Al-Hilal-Obeyed baada ya timu hiyo
kushindwa kucheza mchezo wake wa marudiano wakati CD De Agosto ya Angola
ikifikia hatua hiyo baada ya kufungwa goli moja kwa bila dhidi ya Kaizer Chiefs
kwenye mchezo wakufuzu hatua ya makundi ya klabu bingwa barani Afrika
Nchi ya Angola ni miongoni mwa mataifa ambayo yanatekeleza makatazo na tahadhari dhidi ya maambukizi ya virusi vya corona amabapo kufikia February 10 nchi hiyo imeripoti visa 3262 vya Covid 19 na watu 57 na mpaka sasa wamefariki nchini humo.
Leave a comment