
Waziri
Mkuu wa Tanzania, Kassim Majaliwa amesema kuwa serikali itaendelea kuboresha
maslahi na mazingira ya kazi kwa wafanyakazi tofauti na kuongeza
mishahara.
Akijibu swali la Mbunge wa Konde kupitia chama cha ACT Wazalendo,
Khatibu Said Haji aliyetaka kujujua ni lini serikali itaongeza mishahara kwa
wafanyakazi nchini katika kipindi cha maswali ya papo kwa papo bungeni Dodoma,
Waziri Mkuu amesema kuwa kuna njia nyingi za kuboresha maslahi ya wafanyakazi
ikiwemo kuwapandishamadaraja na kuwapunguzia kiwango cha kodi.
Majaliwa
ameongeza kuwa hakuna haja ya kutangaza nyongeza ya mishahara ya
wafanyakazi hadharani kwani kunaongeza gharama za maisha na kusababisha vitu
vingi kupanda bei bila sababu ya msingi.
"Serikali inaendelea kuboresha maslahi ya watumishi katika maeneo mengine ambayo ni zaidi ya mishahara, na niwaombe wafanyakazi nchini wasikate tamaa kwa kusubiri watangaziwe hadharani," amesema Majaliwa.
Leave a comment