Kwa mujibu wa
taarifa iliyotolewa na Kurugenzi ya mawasiliano Ikulu, Balozi Mhandisi John
William Herbert Kijazi amefariki Februari 17 majira ya saa tatu na dakika kumi usiku
katika hosptali ya Benjamin Mkapa akiwa anapatiwa matibabu.
Taarifa
huyo inaeleza kuwa taratibu za mazishi ya Kiongozi huyo zitatangazwa hapo
baadae.
Lakini Balozi John William Kijazi ni
Nani?
Amekuwa
mwakilishi wa Tanzania nchini India, Singapore, Sri Lanka, Bangladesh na Nepal
mwenye makazi yake jijini New Delhi, India kuanzia mwaka 2007 - 2016 na hivyo
kumfanya kuwa Mkuu wa Mabalozi wote wanaowakilisha Tanzania nje ya nchi.
Kabla
ya kuwa balozi, Mhandisi Kijazi alikuwa Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi na baadaye
Wizara ya Maendeleo ya Miundombinu kuanzia mwaka 2002 hadi 2006, baada ya
kuteuliwa kuwa Balozi ndani ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa
Kimataifa na hatimaye kupangiwa kituo cha New Delhi, India.
Kati
ya mwaka 1996 hadi 2002, Mhandisi Kijazi alikuwa Mhandisi Mwandamizi wa Ujenzi
wa Barabara ndani ya Wizara ya Ujenzi kabla ya kupandishwa cheo na kuwa Mkurugenzi
wa Barabara za Mikoa ndani ya Wizara hiyo hiyo.
Balozi
Mhandisi Kijazi alipata Shahada ya Sayansi ya Uhandisi wa Umma mwaka 1982
kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, na baadaye Shahada ya Uzamili katika
Uhandisi wa Barabara Kuu kutoka Chuo Kikuu cha Birmingham, Uingereza mwaka 1992.
Balozi Mhandisi John Kijazi amefariki akiwa ameacha mke, Fransisca Kijazi pamoja na watoto watatu, David, Emmanuel na Richard Kijazi.
Leave a comment